Yafuatayo ni Madhumuni na Misingi ya Ushirika ya Chama cha Ushirika wa Akiba na Mikopo cha Tazara Mbeya SACCOS LTD
Madhumini ya Chama hiki cha Ushirika ni kuinua na kuimarisha hali ya kiuchumi na kimaisha ya Wanachama wake kwa kufuata misingi ya demokrasia, Kanuni na taratibu za Vyama vya Ushirika kwa kuhamasisha wanachama wake kujenga tabia ya kujiwekea Akiba na kutafuta vyanzo vya Fedha ili kujenga na kuimarisha mtaji kwa ajili ya kutoa Mikopo kwa Wanachama kwa Masharti na riba nafuu. Ili kufanikisha Madhumini haya ya Ushirika huu wa Akiba na Mikopo utafanya yafuatayo:-
• Kupokea na kutunza Akiba na Amana za Wanachama kwa njia rahisi na salama.